Fikiria … unacheza mechi ya mpira wa miguu. Lakini inatokea hakuna mtu anayehesabu magori yaliyofungwa. Je, itawezekanaje kufahamu ni nani mshindi?
Ama unakwenda kwa daktari na anapokuuliza ni “nini kinakusumbua” unashindwa kusema kama ni kichwa, tumbo au mguu wako unauma. Hii itampa wakati mgumu daktari kukutibu.
Kama hujui tatizo, huwezi kupata ufumbuzi wake. Hivi ndivyo ilivyo katika fedha: Ni matumaini yangu kuwa unasoma maelezo haya kwasababu unataka kujifunza namna bora ya kutumia fedha. Jambo la kwanza katika kuboresha namna bora ya kusimamia fedha…inakupasa kutambua juu ya nini unafanyia fedha zako…Kumbuka, utawezaje kukirekebisha kitu kilichoharibika ikiwa haujui mahali palipoharibika?
Jambo la kwanza: Orodhesha matumizi yako yote ya fedha zako – yakiwemo matumizi madogo madogo (kwani huongeza gharama!). Yaani mapato na matumizi ya fedha zako zote.
Tafuta mfumo unaokufaa katika utunzaji wa mahesabu ya fedha zako. Inaweza ikawa programu fulani, ama katika simu yako ya kiganjani, katika daftari au kompyuta; hii inaweza ikafanyika siku kwa siku…Kwa chochote unachojisikia kukifanya yakupasa kukikamilisha. Hakikisha unatafuta kiwango sahihi cha maelezo juu ya kila kitu utakacho taka kukifanya: Mfano: chakula, mavazi au usafiri…ama unaweza ukachanganua zaidi juu ya chakula, kwa kutoa mchanganuo wake kati ya kununulia sokoni ama mgahawani. Hii hutegemea na namna unavyotumia fedha zako. Na kila kitu hutegemea urahisi na umuhimu wake.
Kisha, inapofikia mwisho wa juma jumlisha matumizi yote yanayofanana (mfano: chakula, n.k). kimsingi changanua kama kipato chako ni mshahara wa kila mwezi na ili kupata picha halisi juu ya matumizi yako ya mwezi unaweza kutengeneza mchanganuo huo kwa mwezi mmoja mmoja.
Hebu fikiria…unawekeza katika kampuni kubwa lakini hawawezi kukwambia wanatumia kiasi gani na kama wanatengeneza faida yoyote, je, ungeliwaamini? Hivyo, kuweka kumbukumbu juu ya kila unachotumia ndicho kitu cha kwanza na hukufanya kujiamini. Watu wengi huamini kuwa unapoanza kuweka kumbukumbu ya matumizi yako “hukufungua ufahamu”. “Sikulitambua kumbe natumia fedha nyingi juu ya kitu fulani”. Kumbuka: kama haulijui tatizo huwezi kupata ufumbuzi wake.
Mazoezi:
Yafuatayo ni mawazo ya namna ya kuorodhesha mapato na matumizi yako.
Kitu cha kuzingatia zaidi ni kutumia programu ambayo itarahisisha ufuatiliaji wa kila unachokifanya na kukitumia….kila siku, mwezi baada ya mwezi…ama mwaka mzima!
Mwisho wa somo la kwanza. Furahia ufuatiliaji wa matumizi ya fedha zako hadi somo lijalo!